Tarehe 27 Machi 1979, Mwalimu Julius Nyerere aliwahutubia wananchi juu ya Ujumbe wa Gadafi uliotumwa kwake wakati Tanzania ikiwa katika vita dhidi ya Uganda. Hotuba ile ilipachikwa jina "Saa Ishirini na Nne" na hii nikutokana na kwamba Kanali Gaddafi, ambaye wakati huo alikuwa akitaka kuisaidia Uganda katika mgogoro huo, aliipa Tanzania saa 24 kuondoa majeshi yake katika ardhi ya Uganda. Hata hivyo, Tanzania haikuondoa majeshi yake. Nyerere alimjibu Balozi wa Libya aliyetumwa na Gadafi amfikishie Gadafi hayo maneno. Kwenye hii hotuba Nyerere aliweka wazi nini alimjibu Gadafi. Shukrani za dhati zimwendee Mroki T Mroki aka Father Kidevu kwa kuchapisha nakala ya hii hotuba.